Friday 24 March 2017

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Stephen Kebwe akizungumza wakati wa kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki
Baadhi ya washiriki wa kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki wakifatilia kikao hicho kwa makini
Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo akisikiliza kwa makini wakati wa kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Masharikikilichofanyika Mkoani Morogoro
Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Handeni Mhe Godwin Gondwe akifatilia kwa makini kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki kilichofanyika Mkoani Morogoro, Kushoto kwake ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Ubungo Ndg James Mkumbo
Mkuu wa Wilaya ya Muheza Hajat Mhandisi, Mwanasha Tumbo akichangia jambo wakati wa kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki

Na Mathias Canal, Morogoro

Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Stephen Kebwe ameongoza kikao cha Kamati kuu ya Tathmini na Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo (Nane Nane) Kanda ya Mashariki inayounganisha Mikoa ya Dar es salaam, Tanga, Pwani na Morogoro.

Kikao hicho kilichokuwa na Agenda sita kimefanyika Katika Ukumbi wa JKT Nane Nane Manispaa ya Morogoro ambapo kwa kauli moja kimepitisha Agenda zote sita ikiwemo kupitia Taarifa ya Tathmini ya Maonesho ya Nane Nane 2016 sawia na Taarifa ya Maandalizi ya Maonesho ya Nane Nane ya mwaka 2017 ambayo Kitaifa yanayotaraji kufanyika Mkoani Morogoro.

Akizungumza wakati Akifungua kikao hicho Dkt Kebwe ameitaka kamati inayoratibu shughuli hizo ya TASO kuweka wazi mapato na matumizi ya fedha wanazozipata kwani kufanya hivyo ni kujenga zaidi uaminifu kwa wananchi na kujihuisha kwa pamoja na wadau mbalimbali ili kukuza uchumi nchini kupitia Kilimo.

Dkt Kebwe alisema kuwa TASO kutofanya hivyo ni njia mojawapo ya kuzifanya Halmashauri zingine kutochangia kwa kuhofia fedha zao kutumika pasina weledi uliokusudiwa.

Sambamba na hayo pia amewasihi wadaiwa sugu kulipa madeni yao haraka iwezekanavyo kwani kufanya hivyo itaongeza ustawi na uimara wa Maandalizi ya Maonesho ya Kilimo na hatimaye Kilele chake kuwa na Tija kwa jamii.

Dkt Kebwe amewapongeza wakurugenzi na Wakuu wa Wilaya waliohudhuria katika kikao hicho ambapo alisema kuwa wanafanya kazi nzuri na kuonyesha ushirikiano imara katika Maandalizi hayo japo amesisitiza kuongezwa kwa jitihada za Maandalizi ili Maonesho hayo yawe na weledi na tija.

Sherehe za Maonesho ya Kilimo Nane Nane hufanyika kwa lengo la kuwakutanisha wakulima, wafugaji, na wavuvi kwa kuwaelimisha watazamaji na hasa wakulima, wafugaji na wavuvi kujifunza na kupata uzoefu wa teknolojia na mbinu zinazotumika kuongeza uzalishaji katika eneo la kilimo, Mifugo na Uvuvi.

Katika Maonesho hayo mambo muhimu hutawala ikiwa ni pamoja na kuonyesha mazao mbalimbali sambamba na mifugo mbalimbali kwenye mabanda.

Akizungumza na Mtandao wa www.wazo-huru.blogspot.com Mara baada ya kumalizika kwa kikao hicho Mkurugenzi wa Manispaa ya Ubungo Ndg John Lipesi Kayombo amewapongeza viongozi wote kwa namna ambavyo wanashiriki kuandaa Maonesho hayo huku akisema kuwa pamoja na Halmashauri ya Ubungo kuwa mpya na inaanza kushiriki katika Maonesho hayo kwa Mara ya kwanza atahakikisha kuwa maonesho yanakuwa na tija katika mabanda yote yanayoendelea kuandaliwa na Maafisa Kilimo, Uvuvi na Mifugaji.

MD Kayombo alisema kuwa kupitia Maonesho ya Kilimo mwaka huu 2017 wananchi watapata fursa ya kujifunza mbinu za ufugaji kwa kutumia mabanda bora, Uchanganyaji wa vyakula vya mifugo na ulishaji, Teknolojia bora ya ufugaji wa samaki wengi katika eneo dogo, Utotoleshaji vifaranga kwa kutumia incubator ya kienyeji na kisasa, Uhamilishaji wa samaki na Ng'ombe na teknolojia Nyinginezo.

Akifunga kikao hicho Mkuu wa Mkoa wa Morogoro Dkt Kebwe Stephen Kebwe ambaye ndiye alikuwa mwenyekiti wa Kikao hicho alizitaja changamoto za maandilizi za Maonesho ya Kilimo kuwa ni pamoja na ucheleweshaji wa michango kutoka kwa wadau mbalimbali pamoja na kuchelewa kuthibitisha mialiko kwa wageni walioalikwa kutembelea Maonesho ya Kilimo Nane Nane.
Baadhi ya wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) wakishusha miti tayari kwa ajili ya kuotesha kando ya vyanz vya maji vinavyosimamiwa na mamlaka hiyo.
Kaimu Mkurugenzi wa Mamlaka ya Maji safi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) John Ndetiko akiwa amebeba mti tayari kwa ajili ya kuotesha kando ya chanzo cha maji cha Shiri kilichopo wilayani Hai.
Baadhi ya wanafunzi wa shule za msingi wakisaidia katika zoezi la ubebabji miti kwa ajili ya kuotesha.
Wafanyakazi wa MUWSA wakiwa wamebeba mit kwa ajili ya kuotesha katika chanzo cha maji cha Shiri.
Kaimu Mkurugenzi wa MUWSA,John Ndetiko akiotesha mti katika eneo la chanzo cha maji cha Shiri.
Baadhi ya wafanyakazi wa MUWSA wakiotesha miti katika chanzo hicho.
Hii ni sehemu ya mitiiliyooteshwa Mwaka jana katika eneo hilo zoezi lililooongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimajaro Saidi Mecky Sadicki.
Huu ndio mti uliooteshwa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Saidi Mecky Sadicki katika eneo hilo.
Chanzo cha maji cha Shiri kilichopo wilayani Hai kinachoimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi.(MUWSA.)
Wafanyakazi wa Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira mjini Moshi (MUWSA) wakiwa katika picha ya pamoja mara baada ya kuotesha miti katika chanzo hicho.
Chanzo kipya cha maji cha Mkashilingi kilichopo jirani na chanzo cha chemichei cha Shiri.

Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini.

Wednesday 22 March 2017

Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo, Nape Nnauye (kushoto) na Naibu Waziri wa Utamaduni wa China, Dong Wei (kulia) wakibadilishana mkataba wa makubaliano utekelezaji wa masuala ya Utamaduni baina ya nchi hizo wa miaka mitatu kuanzia mwaka 2017 hadi 2020 katika hafla iliyofanyika Hoteli ya Serena ijini Dar es Salaam leo.





PRESS RELEASE

Afreximbank and TDB Close $500 Million Syndicated Loan Facility for Kenya

Nairobi, 20 March 2017: – The Trade Development Bank (TDB), formerly known as PTA Bank, and the African Export-Import Bank (Afreximbank) today in Nairobi closed a $500 million dual-tranche syndicated loan facility for the Government of Kenya which acted through the country’s National Treasury.
The facility, for which Afreximbank and TDB acted as joint mandated lead arrangers (MLAs), is part of a $1.55 billion debt package of three facilities being arranged and raised in parallel by the National Treasury in the first quarter of 2017.
            The Afreximbank and TDB-led facility comprises two tranches made up of a $200-million 10-year amortizing loan by TDB and a $300-million five-year amortizing loan provided in equal parts by Afreximbank and TDB. The two tranches will be syndicated to development finance institutions.
TDB acted as initial mandated lead arranger, underwriter, documentation bank, joint bookrunner and facility agent for the facility while Afreximbank acted as mandated lead arranger, underwriter and joint bookrunner. Linklaters, London, and IKM, Nairobi, acted as the lenders’ international and local legal counsels while Simmons & Simmons acted for the Government.
           With the closing of the facility the Government successfully completed its $1.5 billion debt raising exercise through the loan market.  The two other facilities are:
·         An $800 million dual tranche 2/3 year facility arranged and underwritten by Citi Bank, Rand Merchant Bank, Standard Bank, and Standard Chartered Bank, which the four MLAs are currently syndicating to commercial banks; and
·         A $250 million two-year syndicated facility arranged and underwritten by TDB, which is also in syndication by TDB.
           With the facilities, the Government of Kenya has achieved unprecedented borrowing benchmarks with new tenors at the 2, 3, 5, and 10 year marks from different investor groups. The MLAs of the $800 million commercial bank facilities successfully stretched the Government’s previous borrowing tenor from two to three years, in line with other blue chip borrowers on the African continent.
By providing five and 10 year financing, Afreximbank and TDB, emerged as market makers, setting new tenor benchmarks for future borrowings by the Government as the longer tenors provide significant additional value to the Government which has been seeking to gradually replace its shorter term liabilities with longer dated ones.
            “This debt raising exercise stands out in more ways than one - as an achievement in the syndicated loan market, as a confirmation of investor confidence for Kenya and as a further step towards better facilitation of inter-African trade,” said Dr. Benedict Oramah, President of Afreximbank. "Afreximbank’s support for the projects to be financed with the proceeds of this facility are consistent with the ‘Deliver’ pillar of our Intra-African African trade strategy which aims to create enabling logistics infrastructure for efficient intra-regional trade."
“Our rebranding represents our rejuvenation and recommitment to innovate and play a more active role in promoting trade, economic development and regional integration. In December TDB approved a USD250M facility to the Government of Kenya, the Bank has played a key role in raising up to USD750M for Government of Kenya in this current Financial Year,” said Admassu Tadesse, President and Chief Executive of TDB. “TDB will continue financing of trade, enterprise and infrastructure, which is evidenced in the tripling of our loan assets in the past two years in Kenya a demonstration of the Banks commitment to the Kenyan Economy”.
Afreximbank and TDB have supported the Government of Kenya and select state-owned enterprises in the past in line with their trade-related mandate of financing trade-enabling infrastructure and their belief that supporting the development of infrastructure, such as roads, ports and energy in Kenya, is key to facilitating trade and creating better access to world markets for landlocked countries in East Africa.

Tuesday 21 March 2017

Monday 20 March 2017

Update: East Africa Crisis Appeal
East Africa Crisis Appeal
This is Ajok, holding a precious piece of paper 
It is a CAFOD and Caritas food voucher, given to her in Yirol, South Sudan.
     
She has exchanged it for beans, wheat, vegetable oil and salt. Food that she hopes will keep her family alive.
     
The UN declared famine in her home area of Unity State, and Ajok’s story is all too familiar; she was forced to flee her home leaving behind all that she has, and is taking care of ten family members.  
     
This emergency food, provided thanks to your donations to the DEC and our East Africa Appeal, really will make the difference between life and death for Ajok and her family – and the thousands of other families we are reaching with aid.
     
Thank you for your compassion and generosity – you are saving lives.
     
Katika hali ambayo haijazoeleka na iliyoonekana kuwa ngeni, Balozi wa Tanzania Mhe. Philip Marmo alimvisha Cheo Kanali Joseph Bakari aliyepandishwa Cheo hivi karibuni kutoka Luteni kanali.
Hafla hiyo fupi iliyohudhuriwa na  ujumbe wa Watanzania waliohudhuria Maonesho ya Kimataifa ya Utalii Jijini Berlin Ujerumani akiwemo Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Rashid Ali Juma, Mshauri wa Rais wa Zanzibar mambo ya Utalii na Utamaduni Mhe. Chimberi Heri, Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania  Mhe. Geofrey Meena, Maafisa wa Ubalozi na wageni wengine ilifanyika karibuni katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania zilizopo Berlin nchini Ujerumani.
Akitoa maelezo mafupi kuhusu tukio hilo  Mhe. Balozi alitanabaisha kuwa kwake ni tukio la kwanza na la la aina yake kupewa dhamana hiyo  na kwamba amepokea maelekezo husika kutoka Makao Makuu ya Jeshi kupitia Wizarani. 
Akisoma sehemu ya maelekezo hayo alisema “ kwa kawaida Afisa anapopanda cheo akiwa nje ya nchi iwapo hataweza kwenda Tanzania kuvalishwa cheo hicho na viongozi husika wa JWTZ, cheo hicho kipya huvishwa na Afisa Mkuu au Balozi wa Tanzania katika Nchi aliyepo”. 
Hivyo, kwa mujibu wa sheria na mamlaka aliyekuwa nayo anatakiwa kumvisha Cheo kipya cha ukanali mhusika kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Tanzania. Kwa mujibu wa maelekezo hayo Kanali Bakari alipandishwa cheo na Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi kuanzia tarehe 31 Januari 2017.
Akitoa nasaha fupi na salam za pongezi kwa niaba ya Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi, wageni waliohudhuria hafla hiyo na Watanzania wote kwa ujumla kwa  Kanali Bakari aliyefuatana na Mkewe Bi Lucy Mlingi, Mhe. Balozi alimkumbusha Kanali Bakari kuwa ni dhahiri kuwa kupandishwa kwake cheo kumetokana na imani ya Mkuu wa Majeshi na viongozi wengine wakuu katika utendaji wake,uadilifu, bidii katika kazi na utii. Hivyo ni vizuri ahakikishe kuwa anafanya kazi kwa weledi,  bidii zaidi na moyo wa kujituma ili kuleta tija na ufanisi zaidi kwa manufaa ya JWTZ, Tanzania na Dunia kwa ujumla. Mwisho aliipongeza familia yake hususani  Mkewe kwa mafanikio hayo na kuwatakia   heri, Baraka na afya njema.
Kanali Joseph Bakari ni mwakilishi wa JWTZ katika Sekretarieti ya Baraza la Michezo ya Majeshi Duniani (International Military Sports Council-CISM) kama Mshauri na msaidizi wa Mkurugenzi wa Michezo katika Baraza hilo.
Baraza hilo liliundwa tarehe 18 Februari 1948 mara baada ya vita kuu ya pili ya dunia. Dhima kuu ikiwa ni kutumia shughuli za michezo na utimamu wa mwili kama njia ya kueneza amani duniani badala ya vita. Baraza hilo lina jumla ya nchi wanachama 134 Tanzania ikiwemo. Miongoni mwa shughuli  za Baraza hilo ni kuandaa mashindano ya michezo ya majeshi ya Dunia.

 Balozi wa Tanzania Mhe. Philip Marmo na  Acting Colonel Joseph Bakari wakisikiliza maelezo kabla ya hatua ya kumvua cheo cha zamani na kumvika kipya
 Balozi wa Tanzania Mhe. Philip Marmo akimvisha cheo kipya Colonel Joseph Bakari 
Balozi wa Tanzania Mhe. Philip Marmo akimvisha kofia ya cheo kipya Colonel Joseph Bakari 
 Balozi wa Tanzania Mhe. Philip Marmo akipikea zawadi maalumu ya  Sekretarieti ya Baraza la Michezo ya Majeshi Duniani (International Military Sports Council-CISM)  toka kwa Kanali Joseph Bakari wakati wa hafla hiyo
 Balozi wa Tanzania Mhe. Philip Marmo akiwa na  Kanali Joseph Bakari na mkewe 
 Balozi wa Tanzania Mhe. Philip Marmo akiwa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Rashid Ali Juma (kushoto)  Mshauri wa Rais wa Zanzibar mambo ya Utalii na Utamaduni Mhe. Chimberi Heri (wa pili kulia) Colonel Joseph Bakari na mkewe 
 Tukio hilo la kuvisha Cheo  lilihitimishwa na kuimbwa wimbo wa Taifa wa Tanzania.
 Picha ya pamoja na ujumbe wa Watanzania waliohudhuria Maonesho ya Kimataifa ya Utalii Jijini Berlin Ujerumani akiwemo Waziri wa Habari, Utamaduni, Utalii na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Rashid Ali Juma, Mshauri wa Rais wa Zanzibar mambo ya Utalii na Utamaduni Mhe. Chimberi Heri, Mkurugenzi wa Masoko wa Bodi ya Utalii Tanzania  Mhe. Geofrey Meena, Maafisa wa Ubalozi na wageni wengine ilifanyika karibuni katika Ofisi za Ubalozi wa Tanzania zilizopo Berlin nchini Ujerumani. Source: Ofisi ya Ubalozi wa Tanzania Berlin Ujerumani