Tuesday 29 September 2015

KAWAIDA


MO dewji
Vinara wa biashara Afrika walipewa tuzo mbalimbali za African Business katika picha ya pamoja. Kuanzia kushoto ni Daphne Mashile Nkosi, Strive Masiyiwa, Helen Hai na Mohammed Dewji . hafla ya utoaji wa tuzo hizo ilifanyika hoteli ya Four Seasons Hotel mjini New York.(Picha na African Business).
Na Mwandishi wetu, New York
MTANZANIA Bilionea Mohamed Dewji amepata tuzo ya Mfanyabiashara Bora wa Afrika wa mwaka 2015, katika kinyang’anyiro cha tuzo za wafanyabiashara bora wa Afrika (African Business Awards 2015).
Dewji  maarufu kama Mo alikabidhiwa tuzo hizo usiku wa kuamkia jana mjini New York.
Katika hafla hiyo iliyofanyika katika hoteli ya Four Season mkabala na jengo la Umoja wa Mataifa (Baraza Kuu) watu wengine waliopata tuzo ni Aliko Dangote, Daphne Mashile Nkosi, Strive Masiyiwa na Helen Hai.
MO alimshinda Aliko Dangote ambao walikuwa kwenye Kategori moja wakiwania tuzo hiyo ya mfanyabiashara bora wa Afrika, huku wengine walioshindanishwa kwenye kategori hiyo ni CEO wa Paramount Group, Ivor Ichikowitz, CEO wa Groupe Loukil, Groupe UADH, Bassem Loukil, na Oscar Onyema DG wa Nigerian Stock Exchange.
Tuzo hizo zimeandaliwa na jarida la African Business .
Pia katika tuzo hizo taasisi kadhaa zinazofanya vyema bara la Afrika zilitambulika. Taasisi hizo ni pamoja na kiwanda cha sementi cha Dangote , Guaranty Trust Bank, Abellon Clean Energy, Nigerian Stock Exchange  na taasisi ya bima kwa masoko yanayochipukia ya BIMA.
Akielezwa wasifu wake katika hafla hiyo, Mo ameelezwa kama mfanyabiashara aliyefanikiwa kutokana na kuongeza kipato na ukubwa wa kampuni ya Mohammed Enterprise toka aitwae kutoka kwa baba yake.
Akiwa mtendaji wa kampuni hiyo, akiwa katika miaka ya 40 amefanya mabadiliko makubwa katika makampuni mbalimbali ya umma yaliyoshindwa kujiendesha katika sekta ya kilimo, viwanda na maeneo ya makazi na viwanda.
Uongozi wake uliwezesha kampuni hiyo ya MeTL kufanya makubwa kiasi cha kumfanya aingie katika jarida la Forbes la matajiri wa Afrika.
Majaji waliompa tuzo  kwa mwaka huu walisema kwamba uongozi wake umewezesha biashara katika kampuni hiyo kuchupa kutoka dola za Marekani milioni 30 hadi bilioni 3.
Akipokea tuzo hizo Dewji alisema kwamba tuzo hiyo ni ishara muhimu kwa waafrika wote na uwakilishi wa uhakika wa vijana katika masuala ya ujasirimali.
DSC_0310
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji.
Tuzo ya Biashara ya Mwaka ilienda kwa kiwanda cha  saruji cha Dangote kinachoongozwa na bilionea wa Afrika, Aliko Dangote.
Kiwanda hiki kilichopo Nigeria kimejipanga kusambaza uzalishaji katika nchi nyingine za Afrika, hatua ambayo imeifanya tuzo hiyo kuwa ya kwao.
Akipokea tuzo hiyo Aliko alisema amefurahishwa sana na tuzo hiyo ya thamani kubwa na kwamba imetolewa wakati ambapo kiwanda hicho kinatanua shughuli zake kuhakikisha ukombozi wa uchumi kwa nchi za Afrika unafanyika kwa dhati.
“Tunaamini katika Afrika. Tunaamini kwamba katika kuhakikisha kuna uwekezaji mkubwa wa miundombinu Afrika itaweza kusonga mbele katika uchumi wake”.
Daphne Mashile Nkosi, Mwenyekiti Mtendaji wa kampuni ya manganisi ya Kalagadi ya Afrika Kusini alipokea tuzo mwanamke bora katika biashara. Majaji walimpa tuzo hiyo kwa kuwa ameonesha mafanikio makubwa katika sekta ambayo kwa kawaida huendeshwa na wanaume.
Mdada huyo anatambulika kwa kuwezesha kupatikana kwa ajira 30,000 huko Northern Cape, na ni muasisi wa mgodi wa aina yake katika kipindi cha miaka 30.
Mfanyabiashara wa Zimbabwe, mjasiriamali, anayependa kusaidia watu wenye mahitaji Strive Masiyiwa alipata tuzo ya mafanikio katika maisha.
CPoF_XCWcAAyCO6
Afisa Mtendaji Mkuu wa Makampuni ya MeTL Group, Mohammed Dewji akipokea tuzo yake.
Strive ambaye ni mmoja wa waanzilishi  na Mwenyekiti Mtendaji kwa kampuni ya kimataifa ya mawasiliano ya simu Econet Wireless amepewa tuzo hiyo kwa mafanikio yake na pia kwa misaada mingi aliyotoa kwa vijana.
Masiyiwa ametumia utajiri wake kusomesha vijana zaidi ya laki moja wa Afrika katika kipindi cha miaka 20.
“Ni heshima kuu kupata nafasi ya kuthaminiwa na jarida lako, Ni heshima kuwa miongoni mwa marafiki… tafadhali endelezeni kazi hii njema,”  alisema akizungumza kwa njia ya video.
Tuzo ya mfanyabiashara wa Mfano imeenda kwa Helen Hai, Mtendaji mkuu wa Made in Africa Initiative.
Tuzo hii kwa kawaida hutolewa kwa mtu aliyetoa mchango mkubwa katika kuboresha hali ya ufanyaji biashara barani Afrika.
Helen ambaye ana asili ya China amewezesha mabadiliko makubwa katika biashara ya viatu ya Ethiopia  baada ya kuanzisha kiwanda cha viatu cha Huajian Oktoba 2011 baada ya kuwa na mkutano na rais wa nchi hiyo Meles Zenawi  mwaka huo huo.
Imeelezwa kuwa kiwanda hicho mara baada ya kuanzisha katika kipindi cha miezi sita tu waliweza kuongeza pato la mauzo ya nje ya nchi hiyo kwa mara mbili na katika kipindi cha miaka miwili kiliajiri waethiopia 4000.
Sasa hivi mdada huyo amefungua kiwanda cha nguo nchini Rwanda.
“Sekta binafsi haikuja Afrika kutoa msaada, tumekuja afrika kufanyabiashara. KLakini katika biashara tunatekeleza maelengo ya maendeleo. Nina imani kubwa na Afrika, naamini kupitia simulizi za mafanikio tunashawishi wengine kujiamini kutwaa uongozi na kuliwezesha bara hili kutambua fursa zake,”  alisema Helen.
Guaranty Trust Bank, iliwashinda wengine kadhaa waliotajwa na  kushinda tuzo ya utawala bora wakati Abellon Clean Energy  ilipata tuzio ya ubinifu wakati Nigerian Stock Exchange ilipata tuzo ya urejeshaji kwa jamii faida ikiwa ni huduma bora za jamii. 
Akizungumzia tuzo hizo ambazo ni za sab, Omar Ben Yedder alisema hafla hiyo imwezeshwa na Zenith Bank, GTBank, Agility na Cofina .
Washindi wa 2015
AFRICAN BUSINESS OF THE YEAR 
-Dangote, Nigeria
BUSINESS LEADER OF THE YEAR
-Mohammed Dewji, CEO, Mohammed Enterprise, Tanzania
MOST OUTSTANDING WOMAN IN BUSINESS
-Daphne Mashile Nkosi, Executive Chairperson, Kalagadi Manganese, South Africa
AWARD FOR GOOD CORPORATE GOVERNANCE
-Guaranty Trust Bank, Nigeria
AWARD FOR BEST CORPORATE SOCIAL RESPONSIBILITY
-The Nigerian Stock Exchange, Nigeria
AWARD FOR INNOVATION
-Abellon Clean Energy, Ghana
INSURANCE COMPANY & INITIATIVE OF THE YEAR
-BIMA ( bimamobile.com )
LIFETIME ACHIEVEMENT AWARD
-Strive Masiyiwa
AFRICAN BUSINESS ICON
-Helen Hai

Monday 28 September 2015

" width="400" />
 Taarifa zinazosambaa kumhusu Mkuu wa Jeshi la Wananchi (JWTZ) Jenerali  Davis Mwamunyange zilizosambaa kwenye mitandao ya jamii kwamba amekula chakula chenye sumu na amekimbizwa jijini Nairobi nchini Kenya kwa matibabu hazina ukweli wowote.Ni uzushi.

Kwa mujibu wa taarifa za familia ya Jenerali Mwamunyange pamoja na makao makuu ya jeshi ambazo Globu ya Jamii imezisaka na kuzipata, kiongozi huyu wa JWTZ hivi sasa yupo nchini Italia kwa ziara ya kikazi ya siku tisa kama anavyoonekana pichani na hajambo kabisa na yu bukheri wa afya.
Hii ni changamoto kwa wakala wa mawasiliano nchini (TCRA) ambayo imekuwa ikilaumiwa kwa ukimya wake wa kutochukua hatua thabiti kuthibiti uongo kama huu kwa kuwatafiti, kuwabaini na kuwachukulia hatua watu kama hawa wenye nia ya kuleta taharuki na machafuko nchini.
Wananchi wengie waliohojiwa na Globu ya Jamii wanahoji endapo kama kweli TCRA ipo na kama ipo ina vifaa vya kisasa iliyodai wanavyo kuwabaini watu kama hawa, na kwa nini hawajafanya kweli toka sheria ya mitandao (Cyber Law) iliyoanza kutumika.
"Endapo kama TCRA watashindwa kumnasa mhusika wa uongo huu wa kuogofya, inabidi mamlaka husika iangalie upya ajira ya watendaji wake maana kama taasisi nyeti kama JWTZ inaguswa na wao wakae kimya tu basi ujue kuna tatizo ambalo inapaswa Serikali ilifanyie kazi", amesema msomaji mmoja wa Globu ya Jamii katika maoni yake.
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjRhqYdCCuQyGy-j1nI-H3JPtWmH3codQHio4o4C8DyB9BIHp1HnqjuE5c2dHtAv9aNtlDtM0WHxKebhYyvHUmRHKvbLVHGjlgcjhLoyLQQgV8g4jcDnXVklsD8ZpEvoCFOPS-19bTPpDI/s1600/unnamed.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;">https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjRhqYdCCuQyGy-j1nI-H3JPtWmH3codQHio4o4C8DyB9BIHp1HnqjuE5c2dHtAv9aNtlDtM0WHxKebhYyvHUmRHKvbLVHGjlgcjhLoyLQQgV8g4jcDnXVklsD8ZpEvoCFOPS-19bTPpDI/s400/unnamed.jpg
" width="400" />


Sunday 27 September 2015

MSAAD TUTANI - USAFIRISHAJI



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgP5buvUN8f6XDPsEAUXU0eshZD9-A6MEmqaJhsxyQjgr742cOzscEyHRpWI012UnjzQMRUvhTEhVioHQjJxWRo9F4tAQTXCr8gZbcUdZqVCF39XVU_q9B0yOcYS359bzEYOUms41A7-C48/s1600/f+1.JPG" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;">https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgP5buvUN8f6XDPsEAUXU0eshZD9-A6MEmqaJhsxyQjgr742cOzscEyHRpWI012UnjzQMRUvhTEhVioHQjJxWRo9F4tAQTXCr8gZbcUdZqVCF39XVU_q9B0yOcYS359bzEYOUms41A7-C48/s640/f+1.JPG
" width="640" />

 Fuso ikipita Njiani kwenye Maonyesho ya "NDIO Fuso ni Faida" jijini Dar, Maonyesho hayo yanatarijiwa kupita kwenye Mikoa kama Tanga – Moshi- Arusha- Mwanza –Shinyanga -Kahama- Dodoma – Iringa – Mbeya  na Songea ambapo shughuli mbali mbali za uchimbaji wa 
madini, kilimo, ujenzi na usafirishaji wa mizigo zinafanyika


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj8g0hleuZEgxnYT5TlsOGuV7WCfB1y7FzVlwgs6eN4ILntkeHJNk_zSiHlcpHEAhXikrdNQK44HcYhzyULVYGTnQq_zh4OVjYn1NqBkEVvL7V1VGI-YGtHOSDUOFDjW67b6Lv2TmcPXgcx/s1600/f+2.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;">https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj8g0hleuZEgxnYT5TlsOGuV7WCfB1y7FzVlwgs6eN4ILntkeHJNk_zSiHlcpHEAhXikrdNQK44HcYhzyULVYGTnQq_zh4OVjYn1NqBkEVvL7V1VGI-YGtHOSDUOFDjW67b6Lv2TmcPXgcx/s640/f+2.jpg" width="640" />

 Wadau wa Usafirashaji wakiwa katika Maonyesho ya 'Fuso ni faida' jijini Dar

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxF7XuPJ8TK3xjxK89z3HUJcLNL2R6St8pYWNs1y0Ac6FiUBUsk7LWpmR7aaoYzpqyIyEcQtjtqjobkbTg4huAF9L0Yo2a4Y5IB3c6jo3ZUqhk_iIe6JnfyhR2pSNxtQjQaKwiB23ty0a9/s1600/f+3.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;">https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhxF7XuPJ8TK3xjxK89z3HUJcLNL2R6St8pYWNs1y0Ac6FiUBUsk7LWpmR7aaoYzpqyIyEcQtjtqjobkbTg4huAF9L0Yo2a4Y5IB3c6jo3ZUqhk_iIe6JnfyhR2pSNxtQjQaKwiB23ty0a9/s640/f+3.jpg" width="640" />

 Wadau wakipata maelekezo ya Huduma ya 'Ndiyo Fuso ni Faida'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjKmQ9k8l06z4sOAh24g9w7wAmcMv9mFekmji-h-LjXz9AoHjK2P-zR4yeWU5N3nGEMz3OfsZNxWyoVru8hHqsnAiZrE0Tjl2J5iWct52qQ1joSbTDU4AULwxj9d6EiX_hAvACF33nD-Cs4/s1600/f.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;">https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjKmQ9k8l06z4sOAh24g9w7wAmcMv9mFekmji-h-LjXz9AoHjK2P-zR4yeWU5N3nGEMz3OfsZNxWyoVru8hHqsnAiZrE0Tjl2J5iWct52qQ1joSbTDU4AULwxj9d6EiX_hAvACF33nD-Cs4/s640/f.jpg" width="640" />


Na Mwandishi Wetu,



Mtandao
 wa miundombinu ya barabara nchini Tanzania inayokadiriwa kuwa na 
kilometa za mraba 91,049 ambayo ni mara 30 zaidi ya mtandao wa reli 
ambayo inaambaa kwenye eneo lenye ukubwa wa takribani kilomita za mraba 
3,682 ikidhihirisha kuwa barabara ndiyo njia kuu inayopendelewa kutumika
 katika usafirishaji wa mizigo.


Usafirishaji
 nchini Tanzania unajumuisha mitandao ya barabara, anga, reli na maji 
ambapo katika njia zote hizi, barabara na reli zinaongoza zikifuatiwa na
 maji na anga.  Hakika katika suala la umbali, mtandao wa barabara za 
Tanzania unashika nafasi ya 51 duniani, kutokana na taarifa 
zilizonukuliwa katika kitabu “ CIA world fact book”


Wakati
 ajali za barabarani zikiendelea kugharimu maisha ya watu, ufanisi wa 
njia hii ya usafirishaji kwa ujumla wake unahitaji kudumisha ubora wa 
usafirishaji wa barabara nchini Tanzania kutokana na ufanisi wake, 
kuokoa mda na kuaminika pamoja na kuchukuliwa kuwa kiunganishi kikubwa 
cha barabara ndogo kwenye barabara kuu za nchi.





Diamond
 Motors limited hivi karibuni wamekuwa katika safari ya kuzunguka 
mtandao huu wa barabara wakihamasisha pamoja na mambo mengine usalama 
barabarani katika kampeni yao ya “Ndio! Fuso ni Faida” Kampeni hiyo 
iliyozinduliwa mwezi julai mwaka huu jijini Dar es salaam ilifika katika
 mikoa ya Tanga-Moshi- Arusha – Mwanza – Shinyanga – Kahama – Dodoma – 
Iringa – Mbeya – na Songea ambapo shughuli mbali mbali za uchimbaji wa 
madini, kilimo, ujenzi na usafirishaji wa mizigo zinafanyika. Pamoja na 
mambo mengine, kampeni hiyo ilidhamiria kujenga uelewa kwa wateja wake 
juu ya jinsi ya kuboresha usafirishaji salama wa mizigo kwa kutumia 
magari ya kisasa zaidi.





Akifafanua
 kwa undani juu ya malori mapya yaliyohusika katika kampeni hiyo ya 
“Ndio! Fuso ni Faida” msemaji rasmi wa kampuni ya Diamond Motors Limited
 ambao ni wadau na wataalamu katika sekta ya usafirishaji wa masafa 
marefu kwa kutumia malori yao ya Fuso alisema soko la Tanzania 
linahakikishiwa malori ya aina ya Fuso FZ na FJ yaliyoboreshwa 
kiteknolojia na kuwa na uwezo wa kuboresha usalama barabarani.  “Malori 
haya yametengenezwa na kitako imara kilichotengenezwa kwaajili ya uzito 
mkubwa na mazingira magumu ya kufanya kazi” alisema Meneje Mkuu (Masoko)
 wa diamond Motors Ltd bwana Laurian Martin.  Aliongeza kusema kuwa 
“tuna nia ya kuborsha sekta ya usafirishaji iliyo bora na salama kwa 
kutumia malori yetu ya Fuso yaliyo boreshwa ki teknolojia”


Alisistiza
 na kusema kuwa “aina mbali mbali mpya za malori yatolewayo na Diamond 
Motors Ltd sio yanaaminiki katika utendaji tu, bali pia yana uwezo 
mkubwa wa ubebaji ambayo ni sifa pekee isiyopatikana katika malori 
mengine ambayo yanalazimika kutumia mafuta mengi ili kukidhi kigezo 
hicho. Kizuri zaidi, malori haya gharama zake za matengezo ni ndogo 
zaidi na hutembea umbali mrefu zaidi wa takribani kilomita 45,000 kabla 
ya kuhitaji matengenezo ya kawaida kama kubadilisha vilainishi”.





Bwana
 Laurian Martin aliendelea kusema kuwa “Sifa hizi ndizo zinafanya malori
 ya Fuso FZ na FJ kuwa suluhisho kamili la usafirishaji na biashara 
nchini Tanzania”. Katika kampeni hiyo mikoa ya kaskazini ikiwemo Tanga, 
Kilimanjaro, na Arusha ilipata  fursa ya kuona faida zinazopatikana 
katika malori haya mbalimbali ya Fuso maboyo ni malori ya ubebaji mkubwa
 yanayopatikana katika kampuni ya Diamond Motors Ltd.  Miji ya mikoa hii
 imendelea kukua katika shughuli za kiuchumi kama vile usafirishaji wa 
mizigo, biashara, viwanda kama vile cementi, malighafi mbalimbali, maua,
 matunda, mazao mbalimbali yatokanayo na miti yanayohitaji kusafirishwa 
kwenda katika sehemu mbalimbali za nchi na nje ya nchi.  Wasafirishaji 
kutoka mikoa hii wameaswa kutumia teknolojia hii ya malori ya Fuso FZ na
 FJ ambayo inaweza kuwapatia Faida zaidi katika biashara zao.





Kampeni
 hiyo pia  ilifika katika mikoa ya Kilimanjaro na Arusha ambayo 
imeunganishwa katika ukanda wa kaskazini na barabara za nchi za jirani 
kama Kenya na Uganda kupitia mipaka yake ya Namanga ikiwa na biashara 
nyingi baina ya nchi hizo zinazopitia njia ya barabara.  Wakazi na 
wafanyabiashara waliohudhulia kampeni hiyo walipata fursa ya kujionea 
sifa zipatikanazo katika malori hayo ya Fuso Fz kutoka Diamond Motors 
Limted ambayo yanauwezo wa kubeba mizigo mikubwa katika mazingira magumu
 katika ukanda huo.  “Ni kwa teknolojia ya kisasa ya magari haya mabapo 
wafanya biashara wanaweza kupata Faida ya biashaza zao kwa kutumia 
malori haya inayotumia mafuta vizuri, ambapo gari hii ina kifaa maalumu 
cha kuzuia mafuta yasitumike endapo gari hii inatembea katika mteremko 
ili kukupa umbali mrefu zaidi kwa mafuta kidogo.


Mikoa
 ya Mwanza na Shinyanga ambayo ni kitovu cha biashara, usafirishaji, 
ushirikano wa kikanda na maendeleo ya kiuchumi katika kanda ya ziwa 
ikiunganishwa na bandari kavu ya Isaka, ilifikiwa na maonyesho haya ya 
Fuso Fz.  Mikoa hii pia inaunganisha nchi jirani za Uganda, Kenya, 
Rwanda, Burundi and Demokrasia ya Kongo ambazo ni nchi zenye biashara 
nyingi kubwa miongoni mwake na Tanzania.





Kwa
 usafirishaji wa masafa marefu katika nchi hizi, Fuso Fz ina muundo 
maridhawa kupasua upepo usiwe kizingiti ambayo haikupatii umbali mrefu 
tu, bali pia inampunguzia dereva uchuvu kwa kuwa na kibini 
iliyoninginizwa vizuri kupumguza sana mtikisiko wa barabarani hasa 
kwenye matuta au barabara mbovu na kupunguza kelele za kutoka kwenye 
injini.  Sifa hii ni muhimu sana kumpunguzia dereva uchovu na hivyo 
kuweza kutosababisha ajali zitokanazo na uchvu wa dereva na kusinzia 
wakati akiendesha. 

Mikoa
 ya nyanda za juu kusini pia ilikuwa katika mpango wa kupata faida 
zitokanazo na matumizi ya malori mapya Fuso Fz yenye teknolojia mpya 
kutoka Diamond Motors ltd baada ya kufikiwa na kampeni hiyo ya “Ndio! 
Fuso ni Faida” Kampeni hiyo ilipokelewa vizuri na wakazi wa mikoa ya 
Dodoma, Iringa, Mbeya na Songea ambapo pia kuna shughuli za kiuchumi 
kama uchimbaji wa madini, kilimo cha chai, misitu na kilimo cha 
kibiashara.  Wafanyabiashara walionyeshwa haja ya wao kubadilisha njia 
za usafirishaji kwa kutumia Fuso Fz na Fuso FJ na hivyo kupunguza 
gharama za uendeshaji na kupata Faida zaidi katika biashara za kiuchumi 
nchini na ukanda wa Africa Mashariki na kati.

HABARI YA AFYA



https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPHaitdjZ6qdAFEHDXoYQICqKbH4nSRxEuvfEbN9mz38jCTqJl6W3YImbQOuwzu13UNaGkr1sOOWx-rRJRrxhK4mfcS9bZ9R0dZ24hgSsdhrG8A9bCy-ErAc2EV8wzZ-bBCDi6F4kSMFDg/s1600/Dr++Revathi.jpg" imageanchor="1" style="margin-left: 1em; margin-right: 1em;">https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiPHaitdjZ6qdAFEHDXoYQICqKbH4nSRxEuvfEbN9mz38jCTqJl6W3YImbQOuwzu13UNaGkr1sOOWx-rRJRrxhK4mfcS9bZ9R0dZ24hgSsdhrG8A9bCy-ErAc2EV8wzZ-bBCDi6F4kSMFDg/s640/Dr++Revathi.jpg
" width="640" />









Na Mwandishi Wetu, 



Ibrahim
 (jina limebadilishwa) alizaliwa nchini Tanzania na alipokuwa na umri wa
 miezi 9 tu alionekana anang’aa na hakuwa na uwezo wa kula na kukua 
vizuri kama watoto wengine wa umri wake. Alikuwa na maambukizi ya mara 
kwa mara na vipimo vya damu vilionyesha upungufu mkubwa wa damu na 
kiwango cha ukosefu wa damu kwa gm 3.5! Ibrahim alikuwa akiishi na chini
 ya robo ya kiwango cha oksijeni kinachohitajika kwenye damu na 
alihitaji haraka kuongezewa damu ili kuokoa maisha yake. Vipimo vya damu
 yake na ya wazazi wake vilithibitisha kuwa alikuwa na thalasemia kuu.





Thalassaemia
 kuu ni hali ya kurithi ambapo huwa na ukosefu wa chembe nyekundu za 
damu. Katika mwili seli shina Uboho huzalisha aina tatu za seli za damu 
katika mwili- nyekundu, nyeupe na chembe chembe za damu. Thalasemia ni 
hali ya kurithi inayoathiri seli nyekundu za damu. Hutokea wakati mtu 
anashindwa kuzalisha kiasi cha damu kinachotakiwa. Mwili wako hautafanya
 kazi vizuri kama chembechembe nyekundu za damu hazizalishi damu ya 
kutosha yenye afya.





Dkt.
 Revathi Raj wa  Hospitali za Apollo Chennai anaeleza zaidi kwamba 
thalasemia ni ya kurithi. Ni kutoka kwa wazazi kwenda kwa watoto kwa 
njia ya jeni. Watu ambao hurithi jeni za damu mbaya kutoka kwa mzazi 
mmoja lakini jeni za kawaida kwa mzazi mwingine wanaitwa kitaalamu 
‘career’. ‘Carriers’ mara nyingi hawana dalili za ugonjwa mwingine zaidi
 ya kuoneshwa upungufu mkubwa wa damu. Hata hivyo, wanaweza kurithisha 
jeni mbaya kwa watoto wao. Watu ambao wana wastani wa kati wa thalasemia
 wamerithi jeni mbaya kutoka kwa wazazi wote wawili. Kama ‘carriers’ 
wawili wakizaa mtoto, kuna 25% ya nafasi ya kuwa na mtoto aliyethirika.


Kwa
 mujibu wa Dkt Revathi Raj madhara ya kuacha thalassaemia bila kutibiwa 
ni pamoja na kushindwa kwa wengu, ini na moyo. Pia, inaweza kusababisha 
mifupa myembamba na migumu na mikunjo usoni. Ni kawaida kwamba watoto 
wasiotibiwa hudumaa ukuaji wa mwili na akili. Watoto wenye Thalasemia 
huwa wanakufa kutokana na moyo kushindwa kufanya kazi na maambukizi 
ikiwa hali hiyo haitatibiwa.


Matibabu
 pamoja na kuongezewa damu mara kwa mara na dawa za kuzuia maambukizi 
huweza kupunguza kasi ya ugonjwa. Watoto wenye thalasemia wanaweza 
kutibiwa kwa kuongezewa damu mara kwa mara. Zoezi hili linatakiwa 
kufanyika kila baada ya wiki 3 au 4 na husaidia kuweka kiwango cha damu 
kawaida. Wakati viwango vya damu vikiwa kawaida mtu anaweza kujaribu 
kuzuia baadhi ya matatizo ya ugonjwa kwa hiyo kuzuia moyo kushindwa 
kufanya kazi na ulemavu wa mfupa na hivyo kupelekea ukuaji mzuri na afya
 kwa ujumla.


Hali
 ya Ibrahim ina maana kwamba wazazi wake walihitaji kusafiri pamoja naye
 kwa zaidi ya km 1,000 kila mwezi kwa ajili ya kuongezewa damu kutokana 
na ukosefu wa vifaa vya kutosha Tanzania. Huku kuongezwa damu 
kulihitajika ili kuendelea kwa maisha yote ya Ibrahim hii ikiwa ni hali 
ya kudumu.





Wangewezaje
 kutoa damu kila mwezi? Kwa nini hakuna mtu aliyegundua kwamba walibeba 
jeni mbovu ambazo zinaweza kuleta madhara kwa mtoto wao? Haya ni baadhi 
tu ya maswali kadhaa ambayo wazazi wa mtoto huyu wanakabiliwa nayo.








Changamoto
 nyingine iliyowakumba wazazi Ibrahim ililikuwa kwamba pamoja na kila 
kuongezewa damu kuna hatari ya madini chuma katika kila kiasi cha damu 
kinachoongezwa. Kujijenga kwa madini chuma husababisha uharibifu wa moyo
 na ini na viungo vingine. Kuepuka, kuzuia au kuchelewesha madini chuma 
kujijenga mtu anahitaji tiba ya madawa kila siku. Kwa bahati mbaya hata 
hivyo, kwa Tanzania tiba hii si rahisi hivyo kupatikana. Maisha kwa 
Ibrahim yalionekana hatarini sana mpaka baada ya familia kusikia kuhusu 
BMT kusaidia kumtibu mtoto wao mdogo na kusafiri hadi Hospitali ya 
Apollo, Chennai nchini India ambako walikutana na Dkt Revathi Raj. 
Hospitali ya Apollo, India ni jina la kuaminiwa katika BMT kwa ajili ya 
wagonjwa wa kimataifa, kama hospitali ina si tu yenye timu ya BMT 
inayosifika, lakini pia masharti magumu sana kudhibiti maambukizi ambayo
 ni muhimu kwa ajili ya wagonjwa wa BMT.


Kwa
 BMT ‘Haematopoietic’ seli shina inapatikana kutoka kwa ndugu ambaye 
hajaathirika anayeendana au mfadhili yeyote na kupandikizwa kwa mtu 
mwenye thalasemia. Kwa bahati mbaya, Ibrahim hakuwa akiendana na 
wafadhili wa familia. Hata hivyo, mfadhili waliyeendana kikamilifu 
katika shina kiini la uboho aliyejisajili nchini India aitwaye DATRI 
alitoa mwanga mpya wa matumaini.


Mkakati
 wa kupandikiza uboho kwa watoto katika Hospitali ya Apollo nchini India
 ina timu ya wataalam wenye ujuzi wa juu na mratibu wa BMT anayefanya 
kazi kama sehemu ya timu ya wataalam mbalimbali kutoa huduma 
iliyoboreshwa kwa ajili ya watoto ambao wanapata tiba ya shina. 
Hospitali za Apollo nchini India zina uzoefu mkubwa nchini humo katika 
kuhudumia watoto wachanga na wadogo wanaoendelea na upandikizaji wa seli
 za shina.





BMT
 ni tiba yenye hatari kubwa ambayo inawezekana kwa asilimia ndogo sana 
ya wagonjwa iwapo mfadhili uboho anayefaa yupo. Hata kama kiwango cha 
mafanikio ya BMT ni sawa na 95%, ni kazi ya hatari na huweza kusababisha
 kifo. Kiwango cha mafanikio hutegemea zaidi iwapo au hakuna uharibifu 
mkubwa uliofanyika kwa kiungo chochote kama vile madini chuma kwenda 
mahali pasipofaa.





Dawa
 mpya katika soko na muendelezo wa ugunduzi katika taaluma ya utabibu 
imewezesha mchakato wa upandikizaji kuwa salama zaidi, hata kwa watoto 
wachanga na watoto wadogo. Hospitali Maalum ya Apollo, imelifanya 
upandikizaji wa seli shina kwa zaidi ya wagonjwa 800 ikiwa zaidi ya robo
 kati yao waliokuwa na thalasemia na zaidi ya kufanikiwa kwa Zaidi ya 
90%.





Ujumbe
 muhimu zaidi mtu anahitajika kuchukua katika hili ni umuhimu wa kupima 
wajawazito. Vipimo vya damu vinaweza kuonyesha kama mtu ana thalasemia 
au ni ‘carrier’ kwa kuwa kinga ni bora kuliko tiba. Dkt Revathi Raj 
katika Hospitali ya Apollo Chennai anashauri kuwa ni bora kumweleza 
daktari wako kumpima mtoto wako kiwango cha ‘ferritin’ cha mtoto wako 
kama ana upungufu wa damu kabla ya maagizo ya vitamini yoyote. Ni jambo 
la kawaida kwa madaktari kutoa maelekezo ya vitamini kwa watoto ambazo 
huonyesha dalili za upungufu wa madini chuma. Hata hivyo, ni muhimu 
kuchunguza tahadhari, kwa maagizo ya kuongeza madini chuma kwa ajili ya 
upungufu wa madini hayo anemia inaweza kuwa sahihi, inaweza kusababisha 
kuzidi kwa madini chuma kwa watoto wenye aina yoyote ya thalasemia. 
Jaribio rahisi kuamua kiwango cha madini chuma, au kiwango cha 
‘ferritin’, katika mwili wa mtu linaweza kufanywa. Kama mtu anaonekana 
kuwa na upungufu wa madini chuma, lakini kiwango cha ‘ferritin’ kipo 
kawaida, pengine wana aina ya kwanza ya ‘beta thalasemia’.





Ndugu
 kuoana mara kwa mara pia husababisha mtu kuwa ‘carrier’ wa thalasemia. 
Ndoa kati ya ndugu ziepukwe kwa kuwa kuna ongezeko la ugonjwa wa kurithi
 na kama inaepukika uchunguzi wa damu kwa wanandoa kabla ya ndoa 
unashauriwa.





Tunahitaji
 pia kuongeza uelewa miongoni mwetu Watanzania juu ya umuhimu wa 
kujitolea kwa kuchangia damu na seli za shina kama msaada kuokoa maisha 
haya. Kuna matumaini kwa watoto wote kupata nafasi ya tiba kwa kuwa kuna
 wengi waliojisajili – hasa watu wazima ili kusaidia wagonjwa wote wa 
thalasemia kuu.








Imechangiwa na:




Dkt. Revathi Raj

Mtaalamu wa magonjwa ya watoto ‘Hematology’, Kupandikiza uboho (BMT)
Apollo Hospitals Chennai