Monday 2 March 2015

RAIS KIKWETE, NAPE, SUMAYE WAHANI MSIBA WA JOHN KOMBA

Mar 1, 2015
 Rais Jakaya Kikwete akisaini kitabu cha mabombolezo, alipofika nyumbani kwa familia na aliyekuwa Mbunge wa Mbinga na Mjumbe wa NEC ya CCM, Marehemu, Kampteni John  Komba , Mbezi Tangi Bovu, Dar es Salaam, leo. Komba mefariki jana katika hospitali ya TMJ Dar es Salaam. Kushoto ni Mke wa Rais Mama Salma Kikwete.
 Rais Jakaya Kikwete akimsalimia mjane wa aliyekuwa Mbunge wa Mbinga, na Mjumbe wa NEC, CCM, Mkurugenzi wa Kikundi cha Sanaa cha Tanzania One Theatre TOT, Kampeni John Komba, Mwalimu, Salome Mwakangale, John Komba, alipokwenda kuhani msiba nyumbani kwa marehemu Mbezi Tangi Bovu, Dar es Salaam.
 Rais Jakaya Kikwete akiwa na Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Nape Nnauye walipokuwa kuhani msiba, nyumbani kwa Kapteni Komba, Mbezi Mbeach, Dar es Salaam
 Nape akisaini kitabu cha maombolezo nyumbani kwa marehemu John Komba