Sunday 30 November 2014

Mrakibu wa Polisi-Captain Kidai Senzala Kaluse enzi za uhai wake. 
Helkopta hiyo ilivyo haribika. 
-- 
 Familia ya Mzee Senzala Kaluse wa Kimara Mwisho Dar es Salaam, inasikitika kutangaza kifo cha mtoto wao KIDAI SENZALA KALUSE kilichotokea Novemba 29, 2014 Saa 4 asubuhi kwa ajali ya Helkopta huko Kipunguni B, Moshi Bar Dar es Salaam.

Mipango ya mazishi inafanyika nyumbani kwa baba yake Mzee Kaluse, Kimara Mwisho. Habari ziwafikie, Ukoo wote wa Warutu, Ukoo wa Kaluse, Ukoo wa Mroki, Familia yote ya Timothy Nathan, Ukoo wa Kajiru na Taluka, Wakamba wote wa Ugweno Msangeni, Bibi wa Marehemu Mary Nathan wa Kinyenze- Morogoro, Familia ya Tarimo ya Ukonga Mombasa, Omary Msuya wa Moshi, Abdalh Mgonja wa Gonja Maore, Hosea wa Arusha.

Taarifa pia ziwafike maofisa wa Jeshi la Polisi Tanzania, Askari wa Kikosi cha Polisi Anga, Ndugu, Jamaa na Marafiki popote pale walipo.

Misa ya kuaga Mwili wa Marehemu itafanyika nyumbani kwao kuanzia Saa 6:00 kabla ya safari ya kuelekea Gonja Maore, Wilaya ya Same Mkoani Kilimanjaro kuanza na mazishi yatafanyika Jumatatu Kijijini Kwao Gonja Maore.  

Mawasiliano zaidi: 
Mroki Mroki- +255 717002303. 
 MATAYO 5: 4 
HERI WENYE HUZUNI; MAANA WAO WATAFARIJIKA